Tuesday, November 2, 2010

HOFU YA MATOKEO KUCHAKACHULIWA, WANANCHI MWANZA WACHOMA MOTO OFISI ZA CCM - NERA



Mara baada ya matokeo ya vituo kuwekwa hadharani, wafuasi wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA, walianza kupita mitaani kwa kushangilia. Lakini muda si mrefu walianza kufanya fujo za kuchoma matairi na hatimae kufikia kuchoma ofisi za CCM eneo la Nera mkoani Mwanza baada ya kusubiri sana kutangazwa rasmi kwa matokeo ya uchaguzi. Sababu kubwa ilielezwa kuwa wananchi hawa walikuwa na wasiwasi kuwa matokeo yangechakachuliwa. Lakini ukweli halisi kutoka eneo la kuhesabu kura zinasema kuwa, kuhesabu kura kulichukuwa muda kwani kila karatasi ilikuwa inapitishwa kwenye mashine ya kuscan ili kuondoa wasiwasi wa kugushi ama kuchakachua matokeo. Wananchi walipaswa kuelezwa haya yote kuepusha vurugu zisizo kuwa za msingi.

No comments:

Post a Comment