Wednesday, October 6, 2010

MWAKA MMOJA BAADA YA KUMALIZA DARASA LA SABA



Vijana hawa wanakusanya mchanga maalumu wa kujengea na kuuza. Mchanga huu unakusanywa katika moja ya mifereji inayopitisha maji machafu kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Mwanza. Eneo hili ni Igoma nyuma ya kiwanda cha Cocacola na karibu kabisa na eneo la mnada wa Ng'ombe. Nilipo wauliza kwanini wako hapa na sio shuleni baada ya kumaliza darasa la Saba? Walinijibu kuwa kuendesha maisha yao wenyewe ni ngumu itakuwaje kuhusu kwenda shule na mahitaji yake... Huyu ndiye mtanzania wa taifa la kesho..

No comments:

Post a Comment