Saturday, September 18, 2010

KIJANA ERICK JACKSON KATIKA DAMPO LA UYOLE-NSAGALA MKOANI MBEYA



Eric Jackson ni kijana mdogo mwenye umri wa miaka 15. Kijana Erick Jackson anaendesha maisha yake ya kila siku kwa kutafuta chuma chakavu katika dampo hili lenye harufu kali na uchafu wa kila aina.
Maisha ya kijana huyu yanaonyesha wazi kua ni magumu kwa binadamu wa kawaida kuishi. Anachokifanya kijana huyu katika dampo hili ni kukusanya vyuma chakavu na baadaye kwenda kuviuza kwa wachuuzi wengine. Erick Jackson anauza vyuma chakavu vyenye uzito wa kilogramu kumi kwa shilingi 1,500.
Inamchukuwa siku nzima kushinda katika dampo hilo ili kupata kilo 10 za vyuma chakavu.
Mtoto Erick Jackson anatumia jembe na mikono yake ambayo haina kinga yeyote kufukua mlundikano wa takataka ili kupata chuma chakavu. Wakati mwingine itamchukua siku mbili mpaka tatu kupata kilo kumi za chuma chakavu. Kwa mantiki hiyo mototo Erick Jackson anatafuta shilingi 500 kwa siku kwa ajili ya kujikimu maisha yake. Je, Mahitaji muhimu ya mwanadamu ambayo ni chakula, malazi na mavazi anayatimiza kwa kiwango gani kama pato lake ni shilingi 500 kwa siku? Maisha ya mtanzania pamoja na kuwa ni umasikini lakini vilevile ni hatari.

No comments:

Post a Comment