Thursday, September 2, 2010

UFADHILI KUTOKA MOIL




Ni faraja iliyoje kwa chama cha mpira wa kikapu mkoani Mwanza MRBA kupata ufadhili wa Trak Suit 30 kutoka kwa kampuni ya ununuzi na usambazaji wa mafuta MOIL iliyo jijini Mwanza. Wadau hawa wamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha mchezo wa mpira wa kikapu unakuwa kwa kutoa misaada mbalimbali. Hivi karibuni timu ya mpira wa kikapu mkoani Mwanza ilisafirishwa na kampuni hii ya MOIL kuelekea Bulyanhulu kwa ajili ya mechi ya kirafiki.

No comments:

Post a Comment