Saturday, September 18, 2010

KIJANA MUSA MARTINI KATIKA DAMPO LA UYOLE-NSAGALA MKOANI MBEYA


Pia katika Dampo hili la Uyole-Nsagala, nilikutana na kijana mwingine anayeitwa Musa Martini, yatima mwenye umri wa miaka 17, Kijana huyu ni mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari ya Uyole day. Yupo katika dampo hili kutafuta makopo ambayo atayatumia kutengeneza vibatari ambapo kila kimoja huuzwa kwa shilingi 150. Nilipo muuliza kwa nini haendi shule na badala yake yupo kwenye dampo hili kukusanya makopo hayo, alinijibu kuwa shuleni anadaiwa ada ya shilingi 15,000 baada ya kulipa shilingi 5,000 kama ada ya mwaka katika shule hiyo. Ada yake ya mwaka ni shilingi 20,000. Musa Martini hulazimika kukatisha masomo yake kwa baadhi ya siku na kuja katika dampo hili kukusanya makopo na kutengeneza vibatari ili kupata ada ya shule. Musa Martini anaishi na mdogo wake ambaye yeye hakupata bahati kufaulu na kuendelea na masomo.
Fikiri kijana Musa Martini atakusanya makopo mangapi na atengeneze vibatari vingapi atakavyo viuza apate ada ya shule pamoja na hela ya kupata mahitaji mengine ya kibinadamu. Kumbuka kibatari kimoja kinauzwa shilingi 150, na je ni vibatari vingapi vitanunuliwa ili apate kuishi? Huyu ndiye mtanzania wa taifa la kesho.

No comments:

Post a Comment